KHOFH

MUNGU, MAISHA YAKE NA, KUSUDI LAKE

MUNGU, MAISHA YAKE NA, KUSUDI LAKE:
NA
Waema J. Mutilu
Hiki kitabu sio cha kuuza. Kimeetolewa pasipo malipo na kanisa la Mungu kwa kuelimisha
uma.
Toloe la kwanza 1999
Kanisa la mungu (C)
Haki yote ihifadhiwe.
Kimechapishwa hapa Kenya.
Uchapichaji wa hiki kitabu umewezeshwa na fungu la kumi na sadaka za waumini wa hii kanisa. Mtu yeyote atakaye kushiriki katika kufanya hii kazi ya Mungu kwa kutoa pesa yake amekaribishwa. Lakini asilazimika. Ni kwa hiari.
DIBAJI
Siku hizi tunasikia mahubiri kila mahali yakitangaza habari za Yesu na wokovu wake. Tumesikia matamshi juu ya kuja kwa ufalme wa Mungu. Ajabu ni hili: hatusikie maelezo kamili kuhusu huu wokovu na hata Yesu mwenyewe. Hatuambiwi maana ya hii tangazo, chanzo chake na hata mwisho wake. Wale wanajaribu kutoa maelezo unena mawazo yao na sio ukweli ulivyo.
Hiki kibatu kinaeleza juu ya asili ya mambo yote – wokovu, dhambi, shetani, mwanadamu, maisha yake na kusudi la Mungu kwetu. Yesu, kulingana na ile injili aliyohubiri, alisema kuwa, alikuja, “… awape uzima wa milele. Na uzima wa milele ndio
huu, wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo vuliyemtuma – Yohana 17:23, “ Alimaanisha nini? Unataka kujua?
Kama ndiyo, fungua akili na uendelee kusoma hiki kitabu huku ukitumia biblia yako kuthibitisha mambo yote tunayoyasema.
MUNGU WA KWELI
Kila mmoja wetu naamini, amewahi kutoka nje usiku wakati hamna mawingu. Umeona mbingu kubwa ambayo imejaa nyota zisizo na hesabu na zenye kung’aa. Sijui kama umewahi kujiuliza;” ni nani aliumbahizi zote?” ijapokuwa ni nyingi hivyo, kila moja ina yake. Hujawahi kusikia zimegongana siku moja; kuonyesha, mwenye kuziumba ana hekima ya juu sana. Tukitoka mawinguni, tunarudi hapa chini ambapo tunaona dunia ilivyo kubwa. Imejaa watu, wanyama, wadudu na uhai wa kila aina. Kila kimoja kina aina yake ya maisha ambayo mahitaji yake yote yanatimizwa. Aliye ziumba ana akili nyingi kiasi ambacho, hakuna kimoja kinasahaulika. Tunao, mwangaza, upepo na maji ambavyo pia viliumba. Ni nani aliyeumba hivi vitu vyote? Hatujawahi kusikia mtu yeyote duniani na hata mbinguni akidai kuumba isipokuwa mmoja tu, naye ndiye huyu Mungu ambaye uzima wa milele unategemea kumjua yeye.
UKUU WA MUNGU
Ukikumbuka vile wengi wanachezea jina na hata neno la Mungu, utakubaliana nami kwamba, watu hawamjui huyu Mungu tunayezungumzia hapa na hii ndiyo sababu kubwa ya hiki kitabu. Umewahi kufikiria wakati wowote kuwa, huyu Mungu ambaye unaapa kwa jina lake na kukataa neno lake iliyo katika biblia niye, “ Mungu aliyeufanya ulimwengu na vyote vilivyomo, ambaye ni Bwana wa Mbingu na nchiMatendo 17:24?
Sikia vile anasema kwa kiywa cha manabii wake. Mbingu zahubiri utukufu wa Mungu, na anga laitangaza kazi ya mikono yake – Zaburi19:1”. Zinahubiri na kutangaza kazi yake kwa njia gani? Ni kwa sababu, hivi na vitu tunaviona kila siku. Tunaona vile vilivyo vikubwa. Hivyo basi vina tushuhudia vile mwenye kuviumba ambaye ni Mungu alivyo mwenye nguvu na hekima kiasi ambacho, hakuna mwingine anaweza kulinganishwa naye. Isaya akishuhudia hayo anauliza; “ ni nani aliyeyapima
maji kwa konzi ya mkono wake, na kuzikadiri mbingu kwa shubiri, na kuyashika mavumbi ya dunia katika pishi, na kuipima milima kwa uzani……..?……. Tazama mataifa ni kama
tone la maji katika ndoo …. Kama si kitu mbele yake … Basi, mtamlinganisha Mungu na nani ? au, matamfananisha na nini – Isaya 40:128?”
Hivyo ndivyo huyu Mungu tunayekujulisha alivyo mkuu na mwenye hekima na nguvu. Mungu ambaye; “ kwa hukumu zake – Zaburi 119:91.” Ni Mungu ambaye anatuuliza hivi:
“ mtanifananisha na nini basi; uziita zote kwa majina, kwa ukuu wa uweza wake; na kwa kuwa yeye ni hodari kwa nguvu zake, hakuna kimoja kisichokaa mahali pake – Isaya 40:2526”.
Umesikia? Yule Mungu tunayekueleza hapa ni yule aliyeumba vitu vyote, na aliye mwenye vyote, hata wewe na mimi tu wake. Ni yule Mungu mwenye nguvu na uwezo juu ya vyote kiasi kwamba, akiamrisha chochote kile (kwa vile vyote ni viumbe vyake), kinamtii.
HUYU MUNGU NI NANI?
Musa alipotumwa na huyu Mungu kwa Ferao ili kumwambia awaachilie waIsraeli, Ferao aliuliza Musa; “ Huyu Bwana ni nai, hata nisikie sauti yake, nakuwapa waIsraeri ruhusa waende zaoKutoka 5:2? Ukisoma hiyo habari katika biblia, utaona kwamba, Mungu hakumjibu Ferao kwa maneno, mbali, kwa vitendo. Alimjibu kwa kumwonyesha vile, ni yeye yule mwenye vyote; mwenye uwezo juu ya viumbe vyote; maana aliamrisha maji, yakageuka kuwa damu. Vyura, inzi na nzige vikatii amri ya Musa. Anga ikamwaga mvua ya mawe, jua likazima mwangaza wake juu ya misri yote. Kupitia kwa hivyo vitendo, alikuwa akimwambia Ferao, yeye ni nani. Kwa hivyo, ikiwa na wewe unataka kumjua huyu Mungu tunayekuhubiria habari zake, basi jua ya kwamba, ni yuyo huyo ambaye aliumba vyote, na mwenye kuamrisha vyote. Ni yule alikuwa tangu milele na hata milele.
Ni yule”…. Munu aliziumba mbingu na nchiMwa 1:1; Ufu 14:7. ni yule aliamrisha bahari ya shamu ikatoa njia kwa wa Israeli. Ni yule ambaye mbele yake, mlima Sinai ulitetemeka, mto Yordani ukarudi nyuma. Ee, tunakuhubiria juu ya Mungu wa Ibrahimu,
Isaka, Yakubu, Mungu wa manabii mabye, baadaye, alimtuma Yesu Kisto akaja kuanzisha kanisa lake ambayo, sisi tunaokuandikia huu ujumbe ni uzao wa kanisa hilo.
Kwa maelezo mengine, ninakuambia hivi;” huyu Mungu ndiye muumba wa vyote – Ni muumba”.
HUYU MUNGU NI NINI?
Tumesikia maelezo mengi ya miungu ya dunia hii ambayo yanatokana na akili za wanadamu, wakiongozwa na shetani kukataa haya maelezo ya huyu Mungu wa kweli ambayo yako katika biblia. Tumesikia wengine wakifundisha habari za Mungu wao ambaye ni watatu katika mmoja. Wengine wanafundisha habari za Mungu mmoja. Basi je, huyu Mungu wa kweli aliye muumba, anajisema kuwa yeye ni nini? Ni watatu ama ni
mmoja ama ni wangapi? Tena, hao wangapi, ni nini?.
MUNGU NI JAMII MOJA
Tunajuaje kuwa jina la Mungu ni jina la jamii? Ili tuweze kuelewa, nilazima turudi katika neno lake ili atueleze yeye mwenyewe. Kitabu cha mwanzo kinaeleza kuwa Mungu ni
muumba lakini tukisoma katika injili ya Yohana tunaona akituambia mambo ya ndani ya huyu Mungu. Hebu tusikie. “ Hapa mwanzo kulikuweko neno, naye neno alikuwako kwa
Mungu, naye neno alikuwa Mungu. Huyo, mwanzo alikuweko kwa Mungu – Yohana 1:12.”
Ningewaomba nyote mnaosoma huu ujumbe, kwanza mtoe yale mafundisho mlio nayo kwa akili zenu, halafu mkubali kuongozwa na biblia, maana biblia ndiyo maelezo ya huyu Mungu wa kweli.
Tukirudi katika kifungu chetu, tunaona wawili ambao wanaitwa kwa hilo jina moja la Mungu. Kumbuka, yohana hapa anaongea juu ya wakati ambao Mungu alikuwa hajaanza kuumba bado. Kwa hivyo, wakati huu, walikuwa hawa wawili peke yao. Swali hi hili; inawezekanaje wawili waitwe kwa jina moja? Tumesikia majina kama Kenya – nchi moja, kanisa moja; jamii ya Yakubu moja n.k. ijapokuwa haya majina yanasimamia kitu kimoja,
utakuta kwamba, ndani ya hicho, kuna vitu vingi. Kwa njia yiyo hiyo, Mungu ni mmoja – ni jamii moja. Mmoja anaitwa NENO. Yule mwingine anaitwa Mungu. Hii ndiyo sababu katika mwanzo unaona hilo jina likitumika kwa umoja, na mahali kwingine, linatumika kwa wingi. Hebu tusikie. “ hapo mwanzoni, Mungu aliumba … Mwa 1:1.” Hapa, Musa anaeleza juu ya hiyo jamii moja. Lakini ukifika kifungu cha 26, jamii hiiyo inaongea yenyewe; ndiyo sababu imeandikwa ; “ Mungu akasema, natuumbe mtu … v . 26.” Wengi wameshanga na kuuliza; “ hapa Mungu (mmoja) anaongea na nani?” Inaweze kanaje Mungu peke yake aseme,” natuumbe”?
Ukweli ni kwamba Mungu ni jamii moja lakini, ndani ya hiyo jamii kuna hawa wawili ambao tumeona katika Yohana – yanii , NENO na MUNGU. Ni hii jamii ya wawili ambayo
ainaonekana ikijadiliana, na kwa vile ni moja, basi Musa, anaripoti akisema, “ Mungu (jamii moja ) akasema, “ Natuumbe” – soma. Mwa 1:26; 3:22. Ikiwa unataka kumjua na
kumwamini huyu Mungu muumba ambaye tunakueleza hapa, elewa kuwa yeye ni jamii moja. Kwa hivyo tunapoongea juu ya jamii, sio makosa kusema Mungu ni mmoja. Likina nje ya huu mpango wa jamii, itakuwa ni makosa, na tena ni uongo kusema, Mungu ni mmoja.: Hii jamii ya Mungu kwa sasa ina hawa wawili ambao tumeona . vile tutaona baadaye, huyu neno ndiye alikuja kuitwa Yesu baadaye na, akaanza kuitwa mwana, huku, huyu Mungu mwingine akianza kuitwa babaona, Yohana14:28.
MAISHA NA NGUVU ZA MUNGU
Hili jamii la Mungu limeishi tangu milele maana, yule neno ambaye ndiye anenaye anasema hivi; “ … kabla yangu, hakuumbwa Mungu awaye yote, wala baada yangu,
hatakuwapo mwingine … tena … “ mimi ni wa kwanza, na mimi ni wa mwisho, zaidi yangu mimi, hakuna Mungu mwingine – Isaya 43:1011; 44:6 “ kwa kuwa huyu Mungu nin wa milele, na maisha yake pia ni ya milele. Akishuhudia hayo, nabii malaki alisema, “ kwa kuwa mimi Bwana sina kigeugeu … Mal 3:6.” Tena, “ jana , leo , na hata milele, ni yeye yuleWaebr 13:8. “hii ni kusema kwamba, maisha ya Mungu ni makamilifu na hayawezi kubadilishwa, maana alisema; ‘ Najua ya kwamba, kila kazi haifanyayo Mungu itadumu milele, haiwezi kuongezewa kitu wala kupunguzwa kitu – Mhubiri 3:14”. Haya nawandikia ili mtu awaye yote asiwadanganye na kuanza kuwapotosha kwa mipango ya wanadamu.
MAANDIKO NI MAELEZO YA MAISHA YA MUNGU
Mungu, huku akikusudia kujidhihrisha kwa wanadamu alinena kupitia kwa manabii (Webr 1:12), kwa yesu na mwishowe kwa mitume. Hayp aliyoyanena ndiyo yaliyo andikwa na kuitwa maandiko matakatifu – soma Isaya 30:8; 1 wakori 10:11; Warumi 15:4; . hii ndio sababu, kila tunaponena kuhusiana na huyu Mungu, tunasema, “ imeandikwa.” Tukisha jua hivyo basi, tunarudi kwa pointi yetu. Mungu anaishi maisha gani?
Mungu kwa maumbile ni roho – Yohana 4:24. Ni jambo la kukubalika basi kwamba, maisha yake ni ya kiroho. Maandiko yanasema kuwa Mungu ni upendo; ni mwema; ni mwaminifu; ni nuru ; ni mileleona 1 Yohana 4:16; Mat 19:17; 1 yohana 1:5; Ufu 2;8. Ukisoma maandiko yayo hayo, utaona kwamba amri za Mungu ni za kiroho, ni upendo, ni njema, ni kamilifu, ni nuru na, ni za milele – ona Warumi 7:14; Warumi 13:10; 7:12; Yakubu 1:25; Zab 1119:105; 8990.
Kile ninachotaka kuwaambi hapa ni, haya maandiko ya biblia ni maelezo ya maisha ya huyu Mungu wa kweli, na kusudi lake la uumbaji. Kwa hivyo, ukitaka kujua chochote kuhusu huyu Mungu na mipango yake, kitafute katika maandiko, maana nje ya hayo, hapana ufahamu wowote wa Mungu. Hii ni agizo kwako
usome biblia sana huku ukiomba sana.
NGUVU ZA MUNGU
Mungu alimpa mwanadamu nguvu za kutenda kazi zake. Mtu utumia hizo nguvu kwa kutembea, kulima, kukata vitu kama miti, n.k. Hizi nguvu za mwanadamu sio mtu mwingine aliye ndani ya mtu, mbali ni uwezo wake wa utendaji. Kulingana na hayo
maelezo, Mungu utumia nguvu ganikutekeleza yote yale anayoyafanya? Malaika walipoasi, dunia ilijaa giza na maji. ( ukitaka maelezo juu ya hili jambo, agiza ujumbe uitwao – “ chanzo cha uasi.” Utatumia ). Tukisoma mwanzo 1:2, maandiko yanasema kuwa; “ … roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.” Hapa, watu walikatta kufuata maagizo ya Mungu juu ya vile wanaweza kusoma na kuelewa biblia – yaani, “… huku
kidogo, na huku kidogo, na huku kidogo – Isaya 28:910,”
wamekosa kuelewa kilichofanya kufunikwa na maji. ( kumbuka kuagiza ujumbe wa “ chanzo cha uasi”) Tukifuatia hilo kanuni la biblia basi, roho ya Mungu ailitulia juu ya maji kufanya nini?
Daudi anatueleza, “ Waipeleka roho yako, wanaumbwa, nawe waufanye upya uso wa nchi – Zab104:30.” Ee, baada ya uharibifu uliosababishwa na uasi wa malaika chini ya
uongozi wa Lucifa, Mungu alianza kuirekebisha dunia, na hiyo alifanya kwa siku sita (Mwa1:326).
Basi, kuambatana na hicho kifungu cha Zabu 104:30, Mungu hutumia roho yake kufanya kazi zake kama vile mwanadamu hutumia nguvu za mwili wake. Hebu tujaribu kuelewa zaidi,” … anga laitangaza kazi la mikono yake – Zab 19:1. “ Tena , “ …
aletaye nje jeshi lao kwa hesabu .. kwa ukuu wa uwezo wake … hodari kwa nguvu zake … Isa 40:2526.”
Ndiyo, Mungu ni roho. Anaposema; “ kuwe nuru” na inakuwa, watu hufikiria hiki kitendo kuwa mhugiza. Hii ni kwa sababu “ mwanadamu wa asili hawezi kuyaelewa mambo ya kiroho – 1 wakori 2:14.” Yesu alishuhudia hayo alipomwambia
nikodemu;” Upepo huvuma upendako, na sauti yake waisikia, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda; kadhalika na hali yake amezaliwa na roho Yohana 3:8.” Eee, tutakapozaliwa mara pili, tutakuwa kama upepo, yaani – hatuwezi kuonekana na watu
wakimwili. Hivi ndivyo Mungu na kazi zake zilivyo kwa mwanadamu wa kimwini. (unataka kuelewa undani wa maana ya “kuzaliwa mara ya pili ?” agiza hicho kitabu naa utatumiwa).
Haya yote nawaandikia ili kuwathibitishia kwamba, roho mtakatifu ni uhai, ni akili, ni uwezo na nguvu za Mungu na sio Mungu mwingine katika uungu. Akishuhundia hayo, yesu alisema; “ maana kama vile baba na Mungu mwana walionao nafsini mwao ni roho mtakatifu. Hii ni kwa sababu maandiko yanasema; “ roho ndiyo itiayo uzima … maneno hayo niliyowaambia ni roho, tana ni uzima – Yohana 6:63;.
Tena, Yesu liahidi kuwatumia roho mtakatifu wote wwaaminio (soma. Yohana 5:26; 4:26). Yohana akiongea kuhusu huyo roho, aliihita “ uwezo wa Mungu, “maana alisema ; “Basi wote waliompokea, aliwapa uwezo wa kufanyika wana wa Mungu – Yohana 1:12.”
Petro anaita hiyo roho, NGUVU ama kipawa, maana yeye pia anasema, “… nanyi myapokea kipawa cha roho… Matendo 2:38.” Yesu alisema atakuwa nasi na kukaa ndani yetu ( Soma. Mat 28:20; Yohana 14:23) yeye na baba. Ni kwa njia ya hii roho yao ambayo inakaa ndani yetu ( som. Mat 28:20; Yohana 14:23) – yeye na baba. Ni kwa njia ya hii roho yao ambayo inakaa ndani yetu. Ona pia – wagal 2:20 . maandiko yanasema kwamba, tunapompokea roho mtakatifu; tuna akili ya Yesu; ndiyo tuna nia ya Mungu tunayekuhubiria juu yake utenda kazi kwa nguvu zake ambazo ndizo biblia inaita “ ROHO mtakatifu.” Ukitaka undani, agiza ujumbe wa “ ROHO MTAKATIFU utumiwa.
KUSUDI LA MUNGU. KWA MWANADAMU
Mungu alipoumba malaika, aliumba pia mbingu na nchi. Zilikuwa nzuri na zakupendeza mpaka malaika walipozitazama, wakafurahi kwa shangwe kuu ( ona. Ayubu 38:7) . Basi,
alipomaliza kuzimba, aliweka theluthi moja ( 1/3 ) ya malaika wake hapa duniani chini ya uongozi wa maliika mkuu aitwaye lusifa, ama “ nyota ya alfajiri, ili waitunze dunia na kuitawala. Huu ulikuwa ni ufalme wa Mungu hapa duniani, ufalme wa kiroho ukitawaliwa na viumbe wa kiroho – Malaika. ( kwa maelezo zaidi, kumbuka kuagiza ujumbe wa: chanzo cha uasi”) – soma pia Ezekieli28:1315. lakini lusifa alishikwa na kiburi na
akawawishi malaika wenzake waipindue serikali ya Mungu; sio hapa duniani tu mbali na hata ile ya mbinguni (som. Ezekieli 28:1717; Isaya 14:13”) . hapo ndipo Mungu alipopinga hilo jaribio la lusifa na kumtupa tena hapa chini . aliuondoa utukufu wake duniani na ufalme wake pia. Ndipo, kama maandiko yasemavyo, ile dunia ilikuwarembo sana, ikajawa na giza na maji, ikawa ukiwa – Mwa 1:2 . lusifa akawa shetani, huku
malaika wenzake wakigeuka na kuwa pepo wabaya. Kuanziia hapo, ufalme wa Mungu ulikoma hapa duniani. Alimwachia shetani na hawa malaika waendelee kuitawala kivyao.
Kwa wale ambao hawajui, hivi ndivyo shetani alifanyika kuwa mfalme na Mungu wa dunia hii. Ni Mungu alimpa kuitawala na hata wa leo, ni yeye amemruhusu aendele kuitwala.
MPANGO WA MUNGU HAUBADILIKA
Maandiko yanatuambia; najua ya kwamba, kila kiazi Mungu aifanyayo itadumu hata milele. Haiwezi kuongezewa kitu au kupunguza kituMhubiri 2:14.” Kwa vile mpango wa Mungu ulikuwa, na hata wa sasa, ni kudumisha vitu vyote kwake alianza kupanga vile atarundisha ufalme wake duniani na kumwondoa shetani pamoja na hawa malaika wabaya.
Aliwaumba malaika wakiwa na uzima ndani yao, na wenye miili ya kiroho isiyoweza kuharibika. Waliopasi, walikomaa katika hayo maisha ya dhambi, huku wakiwa hawawezi kufa. Hii ni kusema kwamba, shetani, na malaika wenzake hawawezi kufa. Hii ni kusema kwamba, shetani, na malaika wenzake hawawezi kufa. Kwa hivyo wataishi hayo maisha ya shida milele na milele – ona 2 petro 2:4; Yuda . 1:6; Ufunuo 20:10. Basi, huku mungu
akikusudia kuimarisha huo uflme tena, aliwazia akijaribu kuona ni nani anaweza kuushikilia pasipo kuasi. Mwishowe, aligundua kwamba ni yeye peke yake ambaye hawezi kubadilika maana yeye ni mtakatifu na wa milele – Yakubu 1:13 . hapa ndipo jamii
ya Mungu ilipanga kujizaa kwa mwanamu. Aliumbwa ili – atawale dunia na baadaye anga yoteona. Mwa 1:27; Zab 8:48;
Waebr 2:89.
Eee, mimi na wewe tuliumbwa ili tuchukue mahala pa shetani na hawa malaika wake. Itawezekanaje, mwanadamu atawale ufamle
wa kiroho – wa Mungu, na hali, mwili na damu haviwezi kuuriti ufalme wa Mungu?
Tukisoma, tunaona kwamba,: Mungu alimfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai na mtu akawa nafsi hai. Hii pumzi ya uhai sio roho mtakatifu kama
vile wengi udhania bali, ni hii hewa tunapumua. Uhai wa mtu wa mwili unategemea hii hewa tunayopumua, maji tunayokunywa, na vyakula tulavyo vikizungushwa kwa mwili wote na damu. Hii nawaandikia mtu awayeyote asidhania kwamba aliumbwa akiwa na roho mtakatifu ndani yake; au afikirie kuwa hii pumzi ya uhai ni roho mtakatifu. Uhai wa huu mwili hutegemea hivyo vitatu.
MWANADAMU AUMBWA HATUA KWA HATUA.
Tukisoma katika maandiko, tutaona Mungu akielezwa hivi; “… mavazi yake yalikuwa meupe kana theluji, na nywele za kichwa chake kama sufu …. Dan 7:9” . hii ni kuonyesha kuwa, Mungu ana nywele za kichwa . Hebu tuone tena. “ kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu … macho kama miali ya moto … miguu kama shaba … sauti … alikuwa na nyote mikononi … Ufunuo1:1416.”
Ninachotaka kuwathibitishia hapa ni kwamba, mwanadumu katika huu mwili ni mfano wa Mungu … aliumbwa akifanana na
Mungu … yani, mwenye kichwa, nywele, macho, mikonona miguu kama Mungu. Hiii ndiyo hatua ya kwanza ya Mungu, ya kuumba mtu ambayo Paulo anbaisema hivi;” lakini hautangulii ule wa kiroho bali, ule wa asili (nyama); baadaye uja ule wa roho – 1 Wakor 15:46,49;” ewe na mimi katika huu mwili wa udongo hatujakamilika bado. Tuko katika sehemu ya kwanza (ama hatua ya kwanza) ya uumbaji wa Mungu kwa mwanadamu.
Kwa vile kusudi la Mungu la kutuumba ni la kujizaa kupitia kwa mwanadamu, ili mwishowe ajiletee wana wengi katika utukifu ( arumi 8:9, Web2:10), Mungu alimpangia mwanadamu miaka elfu sita ya kutimiza huo mpango wa kuzaa (ona Mwa 1:27). Huu pia ulikuwa ni wakati wa mwanadamu wa kujifunza maisha ya Mungu, huku akipinga na kumkana shetani. Kwa nini?
HATUA YA PILI YA UUMBAJI WA MTU
Ijapokuwa mtu aliumba kwa mfano wa Mungu, hukuumbwa mwenye akili ya Mungu wala, hakuumbwa mtuwa kirohokama mungu alivyoroho.Ukikumbuka vile tuliona,baada ya mungu kuumba malaika wa kiroho na wakasi, aliamua kuumba awezaye kusoma na kufa..Ijapokuwamtu aliubwa mkamilieu kimwili, hakuumbwa mwenye ueahamu wa mungu,Mungu ambadilishe na kumfanya mtu wa kiroho nakumpa uzima wa milele.Hii ndiyo ingekuwa hatua ya pili ambayo ni ya kiroho, na ambayo Pauloanainena hivi:\na kama tulivyoichukua sura ya yulewa undogo kadhalika tutaichukua sura ya yeye aliye wa
mbinguni (tutakuwa kirohokama mungu)1wakor. 15:49.
Basi ,ilikuwa mwanandamu achague kwa hiari yake mwenyewe yale maisha angetaka kujifuza ya mungu ama ya shetani, mti waujusi wa mema na mabaya, ama mti wa uzima(kwa maana zaidi , agiza ‘’chanzo cha uasi).
MWANADAMU ATEKWA NYARA NA SHETANI
Ayubu anaonyesha wazi kwamba, ijapowa himo roho ndani ya mwanadamu, ni roho wa mungu impayo ufahamu – Ayubu 32:8. paulo akiongezea pamoja na roho zetu … Warumi 8:6.” Hii ni kusema kwamba, akili ya mwanadamu pasipo roho ingine haiwezi kufahamu chochote.
Basi je, Adamu alichugua roho gani ambayo ilimpa ufahamu wa yule maisha alianza kuishi? Alichagua roho ya Mungu (mti wa uzima)? . Hapana; maana alikula mti wa ujusi wa mema na mabaya yaani; maisha ya shetani. Kwa hivyo, roho yule alimpa ufahamu ni yule wa shetani – ona Waef 2:2. Mungu naye akamtenga naye – ona Mwa3:24. kwa hivyo, Mungu hakuendelea na hii hatua ya pili ya kumuumba mwanadamu kiroho maana shetani alimdangany huyu mtu, akamtega nyara, na kuanza kumfundisha maisha yake.
Kwa hivyo, mwanadamu hakumjua Mungu wala maisha yake. Hii ndiyo sababu nabii Yeremina anasema; “ Eee, Bwana, najua ya kuwa njia ya mwnadamu haimo katika nafsi (akili) yake. Kuelekeza hatua zake sio katika uwezo wa mwanadamu – Yer 10:23.” Ni kwa nini? Isaya anajibu akisema; “lakini, ee Bwana, wewe u baba yetu, sisi tu kazi ya mikono yako – Isaya 64:8”
Ndiyo, sisi bado tunahitaji kukamilishwa katika hii hatua ya pili ya uunambaji ambayo ni ya kiroho. Kama vile hakuna mwingine awezaye kutuumba isipokuwa Mungu, naye hetaniametundanganya tukaa njia za huyo Mung, basi zile njia zetu za kweli hazimo akilini mwetu. Hii ndiyo ile siri ya maisha ambayo huu ulimwengu hauijui (ona 1Wakor2:68).
Eee, watu hawajui Mungu, hawajijui kusudi hii la maisha tumeeleza hapa juu, wala hawajui mwisho wake. Tuseme nini basi? Kusudi Mungu la jujizaa kwa mwandamu na kuimarisha ufalme wake hapa duniani limeshindakana? Sivyo hata kidogo.
MPAONG WA WOKOVU
“ …. kilichozaliwa na mwili ni mwili, na kilichozaliwa na roho ni roho – Yohana 3:6.” Mungu akikusudia kujizaa kupitia kwa mwanadamu, alipanga hatua mbili za kufanya hivyo. Hatua
ya kwanza ni hii tumeona kupitia kwa Adamu ambaye ni mwili na damu. Kwa hivyo, wote wanaozaliwa na adamu ni mwili, maana imeshuhudiwa hivi; “ na kama tulivyochukua sura
ya yule ( adamu) wa udongo… 1 Wakor 15: 49 .” Eee, kama Adamu alivyo mwili, sisi sote tumezaliwa wa kimwili.
Ili uzazi wa kimwili uwezekane, ni lazima yae la mume lishikane na lile la mke; ni lazima mtoto aumbike ndani ya tumbo ya muke kwa miezi tisa; halafu, mtoto uzaliwa akiwa mwili wa nyama kama wazazi wake. (agiza kitabu – KUZALIWA MARA YA PILI ). Hivi ndivyo ilivyo katika uzazi wa kiroho pia. Kama Adamu angekula mti ule wa uzima, yule roho angeunganika na akili yake, ni yule wa Mungu. Hivyo basi , ule ufahamu ambao ungempa namna ya maisha ungekuwa ni akili ya Mungu. Kwa hivyo angeanza kujifunza maisha ya Mungu akiwezeshwa na roho mtakatifu kwa kufuata hiyo roho ya Mungu, angekuwa
tayari anampinga shetani. Hivyo baada ya kukomaa, Mungu angembadilisha na kumpa mwili wakiroho na uzima wa milele. Angekuwa roho kama Mungu alivyo – “ kilichozaliwa na roho ni roho.”
YESU AENDELEA PALE ADAMU ALIANGUKIA
Kwa kuwa adamu hakutimiza kusudi la Mungu, na kwa vile mpango wa Mungu hauwezi kupingwa na yoyote yule; ili aweze kuendelea na hatua yake ya pili ya kuzaa mwanadamu kiroho, alimtuma yesu, ambaye kupitia kwake, tutaichukua surs ya yeye
aliye wa mbinguni – 1Wakor 15:49. umeanza kuelewa maana sasa ya Yesu Kiristo kupitia kwa roho ( mti wa uzima) mtakatifu? – ona . Yohana 6:L63; mithali 3:18; Ufunu22:14 .
Kupitia kwa yesu Kristo, tunapokea roho mtakatifu ambayo inatufundisha kweli (neno la mungu Yohana 17:17; 16:13 ). Kwa kuelewa hiyo kweli, tunaanza kukana uongoona Wef 4:2224.
Wtakaofaulu, Yesu akija, watabadilishwa ( watazaliwa kiroho)na kupewa miili ya kiroho wawe kama baba wao wa kihoro – ona Wafili 3:24; 1Yohana 3:2; na watauingia na kuurithi ufalme wa Mungu na kutawala milele na milele – Dan 7:18;27;12:3. mwishowe, kusudi la Mungu la kujizaa kupitia kwa mwanadamu na kuimarisha ufalme wake hapa duniani litatimia.
Huu ndio ule ujumbe Mungu wa kweli alimtua Yesu aje kutujulisha. Yaani, kumjua Mungu mwenyewe – Yohana 17:3; kusudi lake la kuumba wanadamu – 2 Timo 1:10 na ufalme
wake. Je, utamwamini huyu Mungu wa kweli? Utaiamini hii injili ya kweli? Unayo hamu ya kujua zaidi na ya kuishi kwa kufuata haya maisha yake? Watumishi wake, wako tayari kukuzaidia hata Mungu akukamilishe katika Kristo.